MGCC Front View
KARIBU SANA KATIGA BLOG HII- YOU ARE ALL WELCOME
CFDs National Leadership
MGCC Side to Front View
MGCC Side view

Wednesday, December 28, 2016

Gazeti la Msemakweli Jumapili, Novemba 6-12, 2016, Ukurasa wa 16



Msemakweli
GAZETI LA KIKRISTO LA KILA WIKI
HABARI/TANGAZO
CFDs taifa yazindua kalenda na tovuti

Na Uunique Maringo
Jumuia ya Watetezi wa Imani, The Community of faith Defenders (CFDs) wa Kanisa la Pentecostal Holiness Mission (PHM) imezindua kalenda mpya ya mwaka 2017, tovuti ya Kanisa na blog kwa ajili ya kurahisisha utendaji wa kazi ndani ya makanisa yote ya PHM.
Katika uzinduzi huo uliofanyika Manzese Jijini Dar es Salaama lililopo Kanisa hilo na Mgeni Rasmi ambaye ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Iringa Dakta Given Msomba kwa kushirikiana na Ofisi ya Akofu Mkuu PHM, Baraza la Waangalizi la PHM, Wajumbe wa Bodi ya PHM, Askofu wa Jimbo la Mashariki, wachungaji, wenyeviti wa CFDs Majimbo yote, Dkta Msomba alisema kuwa kutokana na teknologia kukua kwa kasi ni jukumu la kila Kanisa kuachana na mfumo wa analogia na badala yake kuingia katika mfumo wa teknolojia ya digitali ili kurahisisha kazi za kanisa kwenda katika hali inayohitajika.
Alisema kitendo cha Kanisa hilo kuamua kuzindua kalenda mpya ya mwaka 2017 sambamba na kuanzisha tovuti kitasaidia makanisa yote ya PHM ulimwenguni kupata taarifa kwa wakati muafaka badala ya mfumo ule wa awali wa barua ambayo ulikua unachelewa kufikia walengwa kwa wakati.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Iringa, Dk. Given Msomba (kulia) akizindua kalenda ya Kanisa la PHM. Anayefuatia kutoka upande wake wa kulia ni Katibu Mkuu wa CFDs Taifa Bw. Daima Kabogo, Askofu wa PHM Jimbo la Mashariki, Eliya Kiputa na Mwenyekiti wa Taifa, Mchungaji Emmanueli Mwangwale.
Aidha katika risala yao kwa Mgeni Rasmi, Katibu wa CFDs Taifa Bwana Daima Kabogo alisema kuwa tovuti hiyo ya Kanisa inajulikana kama www.phmtz.org na blog ya Idara iitwayo cfdstz.blogspot.com
Katibu huyo alifafanua kuwa CFDs ni Watetezi Imani kama maandiko yanavyosema katika 1Yohana 2:14b kuwa “Nimewaandikia ninyi vijana kwa sabababu mna nguvu na Neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.”
Aliongeza kuwa CFDs wameamua kwa dhati kutangaza Neno la Mungu ulimwenguni kote kwa njia mbalimbali, kianalogia na kidigitali kwa kutumia teknolojia katika kutii agizo la Bwana Yesu Kristo katika Marko 16:15. “Enendeni ulimwenguni mwote mkahubiri Injili kwa kila kiumbe.”
Katibu Kabogo alisema kuwa Idara ya CFDs ina malengo ya jumla ambayo anatamani yafanikiwe ili ufalme wa Mungu upate kujengwa kisha Mungu kujipatia utukufu kupitia kujifunza Biblia, kufanya maombi na maombezi kwa watu wenye shida mbalimbali, kuwasaidia vijana kuishi maisha matakatifu, kushuhudia kueneza Injili na kutoa huduma za kijamii.
Alisema mwelekeo wa Idara ya CFDs ni kuwajibika ipasavyo kwa wana Idara wake kupitia uongozi uliopo ili kuleta maendeleo yenye tija ndani ya Idara yanayolenga ukuaji wa Kanisa la PHM kiroho na kiuchumi kwa kutumia rasilimali zilizopo. Katibu huyo alisema.
Baada ya uzinduzi wa kalenda ya mwaka 2017 iliyotengenezwa na PHM mzaliwa wa kwanza alinunuliwa kwa shilingi laki tatu ambapo wageni waalikwa, wachungaji na watumishi walinunua kalenda hiyo kwa shilingi laki moja
Kalenda hiyo inaendelea kupatikana katika makanisa yote ya PMH.












    Choose :
  • OR
  • To comment
No comments:
Write comments

Popular Posts